HABARI ZA TOWN: siasa

~Jamvi La Habari Na Burudani~

Breaking News
Loading...
Showing posts with label siasa. Show all posts
Showing posts with label siasa. Show all posts

Dr Slaa afunguka haya kuhusu ujio wake Tanzania!!!

Image result for dr slaa
Aliyekuwa katibu mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo, Dkt. Willbroad Slaa amesema hana mpango wa kurudi Tanzania kwa sasa na kwamba taarifa zinazosambazwa hazina ukweli wowote.

Slaa alijiuzulu ukatibu mkuu wa CHADEMA na siasa za vyama baada ya CDM kumpokea Edward Lowassa na kumpa nafasi ya kuwakilisha chama hicho katika uchaguzi wa urais 2015

BUNGE LA TANZANIA LAPOKEA UGENI MZITO HUKO BUNGENI DODOMA!!!

unnamedSpika wa Bunge, Mheshimiwa Job Ndugai (kushoto) akisalimiana na Mbunge wa Bunge la Umoja wa Ulaya Mhe. Alojz Peterle (kulia) pale ugeni wa Wabunge kutoka Bunge la Umoja wa Ulaya ulipomtembelea leo katika Ukumbi wa Spika Mjini Dodoma.ASpika wa Bunge, Mheshimiwa Job Ndugai akizungumza jambo pale ugeni wa Wabunge wa Bunge la Umoja wa Ulaya ulipomtembelea leo katika Ukumbi wa Spika Mjini Dodoma.A 1Spika wa Bunge, Mheshimiwa Job Ndugai akizungumza  jambo pale alipopata ugeni wa Wabunge wa Bunge la Umoja wa Ulaya, katika Kikao kilichofanyika leo katika Ukumbi wa Spika Mjini Dodoma.A 4Spika wa Bunge, Mheshimiwa Job Ndugai (wanne kulia) akipiga picha ya pamoja na Wabunge wa Bunge la Umoja wa Ulaya wakiongozwa na Mhe. David Martin (wanne kushoto) baada ya kumalizika kikao kilichofanyika  leo katika Ukumbi wa Spika Mjini Dodoma.A 3Wageni wa Spika wa Bunge, Mheshimiwa Job Ndugai ambao ni Wabunge wa Bunge la Umoja wa Ulaya wakifwatilia Vikao vya Bunge vinavyoendelea leo Mjini Dodoma.

PROF Jay atema cheche bungeni kuhusu vilio vya wasanii.

Mbunge wa jimbo la Mikumi Mh. Joseph Haule amefunguka na kuitaka serikali kuwekeza fedha za kutosha katika Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo ili wizara hiyo iweze kuwekeza katika sanaa na kuacha kuwatumia wasanii kama makarai ya kujengea.

Prof Jay alisema hayo  Bungeni wakati akichangia makadilio ya mapato na matumizi ya Wizara ya Habari kwa mwaka 2017/ 2018 

"Wasanii wa Tanzania wamekuwa katika mazingira magumu sana na wamekuwa katika umasikini mkubwa licha ya mara nyingi kutumiwa katika kampeni mbambali na hata katika chaguzi zilizopita mmeona jinsi wasanii walivyokuwa wakitumika, mmewatumia kama makarai na baada ya hapo mmeyaweka uvunguni, tunajua makarai huwa yanatumika kwenye kujenga maghorofa na vitu vingine lakini nyumba ikikamilika yanawekwa uvunguni hayatakiwa kuonekana hata kwa wageni" alisema Prof Jay 

Mbali na hilo Prof Jay amesema wasanii wengi wa Tanzania wanakuwa masikini sana sababu wakishatumika huwa hawathaminiwa tena na kuachwa mpaka wakati mwingine wa uchaguzi au kampeni 

Maswali magumu yenye majibu magumu kutoka kwa Lipumba haya hapa!!!

 
Profesa Ibrahim Lipumba, ambaye ana mgogoro na chama chake cha CUF, jana alitinga studio za Clouds TV kujibu mapigo ya hasimu wake, Maalim Seif Sharif Hamad katika kipindi cha 360 na mambo matatu yalijitokeza.
Alichukua hatua hiyo baada ya kipindi hicho cha 360 kumuhoji Maalim Seif juzi na kumsukumia lawama Profesa Lipumba kuwa ndiye anayesababisha mgogoro katika chama hicho, akisaidiwa na Serikali.
File:Ibrahim Lipumba.jpgMaalim Seif, ambaye alimtuhumu Lipumba kuwa msaliti, alisema ni bora kukaa meza moja na CCM kuliko mwanasiasa huyo msomi wa uchumi kwa kuwa chama hicho tawala kinajulikana kuwa adui wa CUF hivyo ni rahisi kuchukua tahadhari.
CUF ipo katika mgogoro baada ya Profesa Lipumba kuandika barua ya kujiuzulu wadhifa wake Agosti 2015 kwa kile alichoeleza kuwa nafsi inamsuta na mwaka mmoja baadaye aliandika barua ya kubatilisha uamuzi huo.
Hata hivyo Mkutano Mkuu wa CUF, uliofanyika Hotel ya Blue Pearl jijini Dar es Salaam, haukukubali Profesa Lipumba kurejea madarakani, badala yake ukakubaliana na barua yake ya kujivua nyadhifa zote, hali iliyoanzisha mgogoro na viongozi wenzake.
Katika mahojiano hayo ya jana, Profesa Lipumba alizungumza na kujibu mambo mbalimbali lakini kati ya hayo, masuala matatu yalikuwa na utata zaidi.
Jambo la kwanza ni pale Profesa Lipumba alipoulizwa na watangazaji wa kipindi hicho sababu za kwenda kuhudhuria Mkutano Mkuu wa CUF uliofanyika Agosti 21, 2016 wakati hakuwa mjumbe.
Lipumba alijibu kuwa aliitwa na baadhi ya wajumbe wa mkutano huo ambao alisema walimtumia ujumbe mfupi wa simu na baadhi kumpigia simu.
“Nilipigiwa simu na wajumbe 12 wakiniambia ‘hapa kwenye mkutano mkuu, barua yako (ya kujiuzulu) inasomwa. Sisi wajumbe tunataka uje uthibitishe hii barua ndiyo yenyewe uliyoandika?” alisema Lipumba.
“Nilipata simu kama kumi au kumi na mbili. Nikaamua kwenda kwenye eneo la Mkutano Mkuu.Niliondoka nyumbani mimi na dereva mpaka kwenye Mkutano Mkuu.”
Maelezo hayo yalimfanya mtangazaji aulize sababu za kwenda kwenye Mkutano Mkuu wakati hajaalikwa na si mjumbe wa mkutano huo.
“Ah! Mimi nimeitwa na wajumbe kwamba hapa unahitajika kuja kuthibitisha,” alisema na kupandishiwa swali jingine.
“Hiyo imekaaje kikanuni. Unapotakiwa kuja kuthibitisha, kikanuni imekaaje. Unaalikwa kwa kutumiwa barua?” aliulizwa.
“Hapana nilitumiwa ujumbe wa simu. Katika taratibu zetu sisi ujumbe wa simu, barua ni utaratibu halali kumualika mtu kuhudhuria kikao,” alisema.
“Sasa sikujua nani ana-chair (mwenyekiti) nani katibu wa kikao kile, lakini nimekwenda kwenye mkutano mkuu. Nimefika eneo la mkutano nimekuta vijana, walinzi wa chama, blue guard, Nimeshuka wamenipokea, wakaniingiza ndani ya ukumbi wa Mkutano Mkuu. Wakanipeleka mahali nikaenda kukaa.”
Alisema alikuta mjadala kuhusu aitwe kujieleza, lakini mwenyekiti (Julius Mtatiro) alikataa na baada ya mapumziko, walipiga kura na kutangaza matokeo kuwa waliokuwa wanamtaka Lipumba ni wajumbe 14 na waliomkataa ni 476.
“Hiki ndicho chanzo cha sokomoko kutokea na kusababisha wajumbe kuimba ‘ni heri ya Jecha (Salim Jecha) aliyefuta matokeo kuliko Maalim Seif kutangaza matokeo wakati kura hazikupigwa’,” alisema Profesa Lipumba.
Jecha ni mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi Zanzibar (ZEC).
Mahojiano hayo pia yalijikita katika sababu za uamuzi wa Lipumba kujiuzulu.
Katika mahojiano hayo, Lipumba alisema aliamua kujiuzulu kwa sababu aliona si sahihi kwa Edward Lowassa kuingia ndani ya Ukawa na kugombea urais na kwamba hakuwa kinara wa kumshawishi Lowassa kujiunga upinzani.
“Ni uongo na mimi nilipata taarifa kutoka kwa (mwenyekiti wa NCCR-Mageuzi, James) Mbatia kuwa Lowassa anahitaji kuzungumza na mimi na hata siku moja sikuwahi kuomba niunganishwe naye,” alisema.
Aliongeza kuwa hata siku moja hakuwahi kuomba namba ya Lowassa.
Alipotafutwa jana, Mbatia alisema hawezi kuzungumza chochote kwa sasa kuhusu kinachoendelea ndani ya CUF.
Juzi, Maalim Seif alisema ana ushahidi kuwa Profesa Lipumba alikwenda kumtafuta Lowassa ajiunge na Ukawa na alimuomba Mbatia amuunganishe naye.
Wakati akimkaribisha Lowassa ndani ya Ukawa Julai 2015, Profesa Lipumba alisema suala la ufisadi ni mfumo na si la mtu mmoja mmoja.
“Sisi tunaponda ufisadi na mfumo wa kifisadi na chanzo kikubwa cha ufisadi ni mfumo ndani ya CCM, kwanza tuing’oe CCM, hapo ndipo tutakapoweza kuondoa ufisadi,” alisema Lipumba wakati wa kumtambulisha Lowassa wakati huo.
“Lowassa alikumbwa na tuhuma za ufisadi mwaka 2008, leo ni 2015 lakini ufisadi umeongezeka au umepungua? Lowassa hayupo serikalini? Tatizo ni mfumo na jambo la kwanza ni kuing’oa CCM.”
Lakini jana, Lipumba alisema kuwa hakusema Lowassa ndiye awe kamanda wa kuongoza vita dhidi ya ufisadi.
Hata hivyo, katika mahojiano hayo Profesa Lipumba alikiri kwenda nyumbani kwa Lowassa na kufanya mazungumzo kuhusu watu wanaomuunga mkono kujiunga na Ukawa.
Alieleza kuwa mipango yote ilisukwa na Chadema na kitendo cha yeye kuhusishwa katika mchakato wa kumshawishi Lowassa ulikuwa ni propaganda.
Alisema hatua yake ya kumlaumu Maalim Seif imetokana na katibu huyo mkuu huyo kufanya vikao na Chadema bila kumshirikisha yeye.
Kuhusu nguvu yake ndani ya CUF, Profesa Lipumba alisema baadhi ya wanachama walimfuata kumshawishi ashiriki kampeni kwa kuwa walimtambua kama bado mwenyekiti.
“Walikuja kina mbunge wa Temeke, Abdallah) Mtolea na (mbunge wa Kinondoni, Maulid) Mtulia kuniomba nishiriki kampeni zao, nikawaeleza siwezi kutokana na hali ilivyo kwa kuwa nitaharibu uhusiano kati yao na Chadema,” alisema
Akizungumzia suala hilo jana, Mtolea alithibitisha kuwa alienda kwa Lipumba kumuomba ahudhurie uzinduzi wa kampeni kama mwanachama wa kawaida.
“Nilimuomba akanikatila kwa sababu ya Lowassa. Nikamweleza mkutano ni wangu mimi siyo wa Lowassa akakataa pia,” alisema Mtolea.
Kuhusu kuwa msaliti, Lipumba alisema “waliosaliti ni wale waliofanya utaratibu wa kumleta Lowassa”.
Sababu za kujiuzulu,
Akizungumzia sababu za kujizulu, Profesa Lipumba alisema ni ukosefu wa umoja ndani ya CUF, hasa baada ya Ukawa kuundwa.
Alisema wakati mwingine, vikao vilifanyika bila yeye kupewa taarifa. “Nikajikuta nina wakati mgumu kulinda maslahi ya umoja na maslahi ya chama na ukosefu huu ulitumiwa na Chadema kuwadhalilisha wagombea wa CUF Bara,” alisema.
Alisema Chadema walisema CUF haina fedha za kusimamisha mgombea na taarifa hizo walipewa na Maalim Seif.
Kuingia ofisini
Profesa Lipumba alisema baada ya Ofisi ya Msajili wa vyama vya Siasa kumtambua kama Mwenyekiti alikwenda moja kwa moja hadi ofisi ya makao ya chama hicho, Buguruni na kukanusha kuwa hakuvamia.
Alisema anamtambua Maalim Seif kama Katibu Mkuu, lakini alishangaa kwa nini hafiki ofisini.
Alisema tayari ameshamwandikia barua ya kuitisha kikao cha kamati tendaji kisha Baraza Kuu la Uongozi.
Aliongeza kuwa hakuanza kutofautiana na Maalim Seif baada ya kujiuzulu bali wakati wa mchakato wa maoni ya Rasimu ya Katiba mpya.
Alisema Maalim Seif alitaka muungano wa mkataba wakati msimamo wa chama ilikuwa ni Serikali tatu.
CUF ina wabunge 42, na kati ya hao ni wawili tu wanaomuunga mkono Profesa Lipumba

Mzee Mkapa asema haya kuhusu serikali ya Magufuli na sakata la vyeti feki!!!

Image result for mkapa
Rais mstaafu wa awamu ya tatu wa Tanzania, Benjamin Mkapa kwa mara ya kwanza amezungumzia utawala wa Rais Dkt John Pombe Magufuli huku akimpongeza utendaji kazi wake unavyokwenda.

Rais Mkapa alimpongeza kwa kufanikisha zoezi la kuondoa wafanyakazi hewa na wenye vyeti vya kughushi vya taaluma na kazi, na akasema anasikitika tu kwamba kwa nini yeye hakufanya hivyo wakati wa utawala wake.

Mzee Mkapa aliyesema hayo alipokuwa akifanya mazungumzo yake na Shirika la Habari la Ujerumani (DW) ambapo miongoni mwa mambo mengi aliyozungumzia ni utawala wa Rais Magufuli, uhuru wa vyombo vya habari, masuala ya uchumi.

Alisema Mkapa kuwa, wenye vyeti feki au watumishi hewa walikuwa wakiingizia serikali hasara wengine wakiendelea kukaa madarakani bila ya kustaafu, hivyo lilikuwa ni jambo la lazima kufanyika ni kwa manufaa ya taifa.

“Masikitiko yangu pekee ni kwamba kwa nini sikufanya uhakiki huu wakati nikiwa madarakani. Labda nilikuwa na mambo mengine makubwa zaidi niliyotakiwa kuyafanya lakini kwa hili alilofanya Magufuli namuunga mkono kabisa,” alisema Mkapa.

Kauli hii ya Rais Mkapa imekuja ikiwa ni siku chache baada ya Rais Dkt Magufuli kuwaamuru watumishi wa umma 9,932 waondoke kwenye utumishi wao baada ya kubainika kughushi vyati vyao.

ZITTO AFUNGUKA HAYA MAZITO KUHUSU MDEE!!!

Mbunge wa Kigoma mjini, Zitto Zuberi Kabwe, ametoa shukrani kwa Bunge la Tanzania kwa kumsamehe Mbunge wa Kawe, Halima Mdee kwa kuendelea na vikao vya Bunge.

Mbunge Zitto ametumia ukurasa wake wa Facebook kutoa shukrani hizo kwa bunge. Ameandika hivi:

 Hatimaye Waziri Kivuli wa Fedha ndg. Halima Mdee amesamehewa na ataendelea na vikao vya Bunge. Hii ndio haki. Mtu aliomba radhi hadharani, kwanini aadhibiwe. Shukran Kwa Bunge.

Halima Mdee alituhumiwa kutumia lugha chafu bungeni wakati wa uchaguzi wa Bunge la Afrika Mashariki, Aprili 14 mwaka huu.

NDOTO ZA MAGUFULI KUTIMIZWA!!!

Image result for magufuli
WATANZANIA wameshukiwa na neema katika mwaka huu wa fedha kutokana na Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano kupanga kuunganisha mikoa yote nchini kwa kujenga barabara za lami na madaraja.

Bajeti hiyo ni ya neema pia kwa wakazi wa Dar es Salaam kutokana mkoa huo kupangiwa kiasi kikubwa cha fedha kwa ajili ya kujenga barabara za lami nyingi, za viungio na za juu kwa ajili ya kupunguza msongamano wa magari jijini humo na katika majiji na mji mikubwa mingine.

Bajeti hiyo ya mwaka 2017/18 ya Sh trilioni 4.5 imeweka vipaumbele katika kukamilisha miradi inayoendelea, miradi inayofadhiliwa na washirika wa maendeleo kwa miaka mitano 2016/17 hadi 2020/21, kutekeleza ahadi za ilani ya CCM ya Uchaguzi Mkuu 2015 na ahadi za viongozi wa serikali walizotoa wakati wa kampeni za uchaguzi mwaka juzi.

Akisoma bungeni jana, Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Profesa Makame Mbarawa alisema, bajeti hiyo ya ukombozi kwa maana ya kuwa inalenga kuunganisha mitandao ya barabara nchini ambayo ni muhimu katika kujenga uchumi wa viwanda.

“Bajeti hiyo iliyotengwa katika sekta tatu za wizara hiyo, sekta ya ujenzi itatumia Sh trilioni 1.9 wakati sekta ya uchukuzi ambayo imeongoza kwa kuombewa fedha nyingi inaomba kupewa Sh trilioni 2.6 na mawasiliano Sh bilioni 18.1,” alisema.

Waziri huyo alisema, kati ya fedha hizo, trilioni 2.6 zilizoombwa kwa ajili ya sekta ya uchukuzi, kiasi cha Sh bilioni 900 zitatumika katika kujenga Reli ya Kati sehemu ya Dar es Salaam hadi Dodoma kwa kiwango cha standard gauge.

Profesa Mbarawa alisema, pia Sh bilioni 500 zitatumika katika kampuni ya ndege kwa ajili ya kukamilisha malipo ya ununuzi wa ndege tatu ambapo mbili za aina ya CS 300 zenye kubeba abiria 127 kila mmoja na moja ya masafa marefu aina ya Boieng 787-8 Dreamliner yenye uwezo wa kubeba abiria 22.

Kuhusu Sekta ya ujenzi iliyotengewa Sh tril 1.9, Prof Mbarawa alisema Sh bilioni 12.8 zitatumika kwa ajili ya kufidia ili kupata eneo kwa ajili ya ujenzi wa barabara ya Dar es Salaam- Chalinze Km 144, ujenzi ambao utakuwa wa ushirikiano baina ya serikali na sekta binafsi (PPP).

Waziri Mbarawa alisema, kati ya fedha za sekta hiyo, Sh bilioni 30, zitatumika katika kujenga barabara za mikoani na madaraja ikilenga katika kuunganisha mikoa yote Tanzania kwa barabara za lami.

“Kazi zilizopangwa kutekelezwa ni ukarabati wa km 469.5 kwa kiwango cha changarawe, kujenga km 58.4 kwa kiwango cha lami na madaraja 12,” alisema. Alisema kati ya fedha hizo, Sh bilioni 46.9 zimetengwa kwa ajili ya kuendelea na ujenzi wa flyover ya Tanzania, Interchange ya Ubungo pamoja na upembuzi yakinifu na usanifu wa kina kuboresha barabara za makutano.

“Barabara hizo ni iliyopo eneo la Kamata, Magomeni, Mwenge, Tabata/Mandela, Morocco, Buguruni, Makutano ya barabara za Kinondoni/ Ali Hassan Mwinyi na Kenyatta na Selander zinapokutana barabara ya Mwinyi na Umoja wa Mataifa (UN),” alisema.

Alisema, pia fedha hizo zitatumika katika kuboresha viwanja vya ndege kikiwamo cha Kimataifa cha Kilimanjaro kilichotengewa Sh bilioni 32.6 kwa ajili ya upanuzi wa barabra ya kuruka na kutua ndege.

“Fedha zitatumika kujenga maegesho ya ndege, barabara za viungio, jengo la abiria na ujenzi wa barabara mpya ya kiungio, usimikaji wa taa za kuongozea ndege na ujenzi wa mfumo mpya wa majitaka,” alisema.

Profesa Mbarawa alisema, Uwanja wa Ndege wa Kimataifa cha JNIA umetengewa Sh blioni 35 kwa ajili ya kuendelea na ujenzi wa jengo jipya la abria terminal III na miundombinu yake.

Sekta ya mawasiliano imepata Sh bilioni 18.1 kidogo ukilinganisha na sekta nyingine mbili, fedha hizo pia zitatumika katika kuendeleza ujenzi wa mkongo wa Taifa hadi katika makao makuu ya wilaya zote nchini.

“Zitatumika pia katika ujenzi wa vituo viwili vya kutunza data kimoja Dodoma na kingine Zanzibar pamoja na kuwezesha uwekezaji wa viwanda nchini,” alisema. Kuhusu Mfuko wa Barabara, Waziri Mbarawa alisema, unatarajia kukusanya Sh bilioni 917.5 ambazo zitatumika katika kufanya matengenezo ya barabara nchini, katika fedha hizo sekta ya ujenzi imetengewa Sh bilioni 642.3 na ofisi ya Rais Tamisemi Sh bilioni 275.2.

Kati ya Sh bilioni 642.3 zilizotengwa, Sh bilioni 573.1 kwa ajili ya Tanroads na Sh bilioni 63.7 kwa ajili ya sekta ya ujenzi kufanya matengenezo ya barabara za wizarana Sh bilioni 5.52 kwa ajili ya uendeshaji wa Bodi ya Mfuko wa Barabara.

Mbarawa alisema, miradi ya barabara kuu itaendeshwa kutokana na fedha kutoka mfuko wa barabara, ambapo Sh bili 16.3 zimetengwa kwa ajili ya kufanya upembuzi yakinifu na usanifu wa kina kilometa 3,624.8.

“Miradi ya barabara za mikoa imetengewa Sh bilioni 33.9 kutoka katika mfuko wa barabara, fedha hizo zitafanya kazi ya ukarabati wa barabara kilometa 688.3 kwa kiwango cha changarawe na kujenga kilometa 40.6 kwa kiwango cha lami na madaraja 12,” alisema.

Waziri Mbarawa alisema, jumla ya Sh milioni 573.1 kutoka mfuko wa barabara zitatumika kwa ajili ya matengenezo ya barabara kuu, barabara za mikoa, madaraja uendeshaji mizani, gharama za usimamizi na uendeshaji wa wakala wa barabara.

MSIGWA AGEUKA MBOGO BUNGENI DODOMA!!!

Mbunge wa Iringa Mjini (Chadema), Mchungaji Peter Msigwa 

Dodoma. Mbunge wa Iringa Mjini (Chadema), Mchungaji Peter Msigwa ameitaka Serikali ieleze sababu za kuwatumbua watumishi bila ya kuwapa nafasi ya kujitetea.

Hata hivyo, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais (Utumishi na Utawala Bora) Angella Kairuki alikana madai hayo akisema hakuna mtu anayetumbuliwa bila ya kufuata utaratibu.

Katika swali la nyongeza, Msigwa alitaka kujua haki za watumishi wanaotumbuliwa kwa kile alichokiita kwa mafungu, lakini bila ya kuwapa nafasi ya kujitetea.

Pia, alihoji wanatakiwa kutafuta haki yao wapi hata kama wametumbuliwa na Rais.

Katika swali la msingi, Mbunge wa Viti Maalumu (Chadema), Ruth Mollel alitaka kujua ikiwa Tanzania inaongozwa kwa kuzingatia Katiba, sheria na kanuni ni kwanini baadhi ya watumishi walioajiriwa wamekuwa wakisimamishwa kazi na Rais, wakuu wa mikoa na wilaya bila ya kuzingatia sheria ya utumishi wa umma na kanuni zake.

Akijibu, Waziri alisema kanuni za utumishi wa umma hutekelezwa kwa kuzingatia katiba, sheria, kanuni, utaratibu na miongozo na kwa mujibu wa ibara ya 36 ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano ya mwaka 1977, Rais ndiye mwenye mamlaka ya mwisho kuhusu usimamizi na uendeshaji wa utumishi wa umma.

Alisema ibara ya Katiba imempa uwezo Rais wa kukasimu madaraka mbalimbali kwa ndani ya utumishi lakini kukasimu huko hakuwezi kutafsiriwa kuwa Rais hana mamlaka hayo tena kama ilivyofafanuliwa katika ibara 36 (4) ya Katiba na Kifungu cha 21 (4) na Sheria ya Utumishi wa Umma Sura ya 298.

Kairuki alisema hata watumishi waliofukuzwa au kusimamishwa kazi na Rais, wana nafasi ya kukata rufaa kwa mamlaka zingine na ikibainika kuwa walionewa, watapewa haki yao.

Katika majibu ya nyongeza, Waziri wa Nchi Ofisi ya Tamisemi, George Simbachawene alisema wakuu wa mikoa na wilaya wanayo mamlaka lakini wanapotoa uamuzi wa kuwasimamisha kazi watumishi, huwa si mwisho bali wakurugenzi ndiyo hutakiwa kuchukua hatua au makatibu tawala wa mikoa.

RAIS SHEIN AWEKWA KITIMOTO BUNGENI DODOMA!!!

MSEMAJI Mkuu wa Kambi rasmi ya Upinzani bungeni, Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano), Ally Saleh jana alisusa kuendelea kusoma hotuba yake kwa madai kuwa hakuna uhuru wa kujieleza katika chombo hicho cha kutunga sheria.

Saleh alikatiza hotuba hiyo, baada ya kutakiwa kufuta kauli iliyohoji uhalali wa Dk. Ali Mohammed Shein kukalia kiti cha Rais wa Zanzibar.

Mwanasheria Mkuu wa Serikali( AG), George Masaju alisema maneno yaliyotamkwa na Saleh hayapo katika uhalisia.

Masaju alisema Saleh anapaswa kurekebisha kauli yake kwa sababu Rais Dk. Shein alishinda uchaguzi mkuu uhalali.

Kufuatia ushauri wa AG, Mwenyekiti wa Bunge, Mussa Hassan Zungu alisema maneno yaliyomo katika hotuba ya upinzani yaliyosomwa na mbunge Saleh ni lazima ayatoe kwa sababu siyo maneno sahihi na hayapo katika uhalisia.

“Kwa hiyo maneno katika ukurasa wa tatu, kwenye namba tatu inatoka, kwa Dk. Shein inatoka kwa sababu alichaguliwa kihalali, ukurasa wanne wote," alisema Zungu.

Hata hivyo Mbunge Saleh aliamua kuondoka bila ya kuendelea kusoma hotuba hiyo na kusema kuwa uhuru katika bunge hauko kiasi cha kutosha.

Mbali na kuhoji uhalali wa Rais wa Zanzibar, wakati akisoma hotuba hiyo Saleh alidai wizara zinakiona cha moto, mawaziri wamebanwa mbavu na kwamba muungano siyo ajenda ya awamu ya serikali ya awamu ya tano kutokana na matendo ambayo yanatokea.

Alisema endapo hali hiyo itaendelea basi "kidagaa kitamuozea mtu mkononi na maiti atampakata yeye."

Mara baada ya kusoma sehemu hizo katika hotuba yake, ndipo Mwanasheria Mkuu Masaju aliposimama na kutoa taarifa na kusema kuwa Saleh anatumia maneno ambayo ni makali.

Masaju alisema Saleh anapaswa kurekebisha kauli kwa sababu hakuna wizara iliyokiona cha moto wala waziri aliyebanwa mbavu, pia Rais Dk. Shein alishinda uchaguzi mkuu kwa uhalali.

Kauli hiyo ya Masaju ilizua tafrani bungeni hali iliyosababisha baadhi ya wabunge upinzani kusimama na kuomba taarifa.

Mbunge wa Kawe (Chadema), Halima Mdee alisema Mwanasheria Mkuu Masaju anapoteza muda kwa kuwa anazungumzia masuala ambayo hayapo kikanuni.

Naye Mbunge wa Iringa mjini (Chadema), Peter Msigwa alisema uhuru wa kambi ya upinzani upo kikatiba.

Alisedma bunge linaendeshwa kwa kanuni hivyo walio wachache wasikilizwe na walio wengi wanapswa kutoa maamuzi.

“Sasa Serikali hata sisi tuliowachache tunavyotoa maoni na mawazo tunazuiwa, hivi utamaduni wa bunge hili ni upi? AG badala ya kuisaidia Serikali ili inyooke amekuwa mtetezi, na bado anapotosha hapa," alisema Msigwa.

"Sisi ni upinzani na ndiyo kazi yetu, sasa kama kila kitu tunachoandika tunapingwa, mnataka tufanyeje? Hatujaja hapa kuwasikiliza nyie.”

FEDHA KIDOGO
Wakati akisoma taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Viwanda, Biashara na Mazingira kuhusu utekelezaji wa majukumu ya hifadhi na usimamizi wa mazingira katika ofisi ya Makumu wa Rais, mjumbe wa kamati hiyo Marry Mwanjelwa alisema ofisi hiyo ilipewa fedha kidogo kulinganisha na maombi ya mwaka 2016/17.

Alisema kati ya Sh. bilioni 20.3 zilizoidhinishwa na bunge kwa mwaka 2016/17 kwa matumizi ya ofisi ya Makamu wa Rais Mazingira hadi Machi 15 ni Sh. bilioni 7.79 tu zilikuwa zimetolewa.

Awali wakati akiwasilisha bungeni makadirio ya mapato na matumizi kwa mwaka wa fedha 2017/18, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais, January Makamba aliomba bunge kuidhinisha makadirio ya matumizi ya Sh. bilioni 15 kwa ajili ya wizara yake.

Kadhalika alisema kwa mwaka 2017/18 ofisi ya Makamu wa Rais Mazingira iatendelea kuratibu mashirikiano yatakayoiwezesha Zanzibar kujenga uwezo na kunufaika katika shughuli za uchimbaji wa gesi na mafuta.

Alisema katika mwaka 2016/17 Serikali ya Mapinduzi Zanzibar (SMZ) imeendelea kupokea fedha kutoka Serikali ya Muungano wa Tanzania, na kwamba hadi kufikia mwezi uliopita Sh. bilioni 1.4 za mfuko wa maendeleo ya jimbo na Sh.bilioni 15.75 za kodi ya mishahara zilipokelewa na SMZ.

IKULU;RAIS MAGUFULI AFANYA UTEUZI HUU MWINGINE!!!

Rais John Magufuli amemteua Profesa Raphael Chibunda kuwa Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo (SUA).

Taarifa iliyotolewa na Katibu Mkuu Kiongozi Balozi John Kijazi, Ikulu Jijini Dar es Salaam jana imeeleza kuwa uteuzi wa Profesa Chibunda unaanza jana tarehe 24 Aprili, 2017.

Kabla ya uteuzi huo Profesa Chibunda alikuwa Mkurugenzi Msaidizi, Idara ya Sayansi na Teknolojia katika Wizara ya Elimu, Sayansi, Teknolojia.

Profesa Raphael Chibunda anachukua nafasi ya Profesa Gerald Monela ambaye amemaliza muda wake.

Wakati huo huo, Rais Magufuli amewasili mjini Dodoma ambako pamoja na mambo mengine atakuwa mgeni rasmi katika sherehe za maadhimisho ya miaka 53 ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar.

MBUNGE WA TEMEKE ASEMA HAYA MAZITO KWA PROF LIPUMBA HADI AIBU!!!

Mbunge wa Temeke Mh. Abdallah Mtolea amefunguka na kudai kuwa aliyekuwa Mwenyekiti wa CUF Prof . Ibrahim Lipumba ni msomi ambaye amejishushia heshima kwa kufanya jambo la ajabu  la kuagiza vijana wake kuvamia mkutano wa CUF.

Mh. Mtolea amefunguka hayo alipohojiana na EATV  na kudai kuwa Lipumba amefanya vitu vya ajabu ambavyo jamii iliyokuwa inamuheshimu sasa itampuudha na yeye atapunguza heshima aliyoitengeneza kwa muda mrefu.

"Mimi Lipumba ni kama kaka yangu kwa jinsi nilivyokuwa namuheshimu, lakini pia alikuwa kiongozi wangu bado namheshimu ila kwa kitendo kilichofanyika pale VINA nimeishusha heshima yangu kwake kwa kiasi kikubwa sana na niseme tu amekuwa mtu wa ajabu sana, elimu yake yotee na heshima aliyonayo amekuja kuiharibu kwa mambo ya ajabu kama yaliyofanyika"- Mh. Mtolea alifunguka.

Aidha katika hatua nyingine Mh. Mtolea amekiri kusikitishwa na kitendo cha jeshi la polisi kuzuia mkutano wake uliopangwa kufanyika  jana kujadili jinsi ya kuzitatua kero za wananchi na kuhusisha mkutano wake na masuala ya kisiasa kitu ambacho kinaweza kurudisha maendeleo nyuma.

" Ni kweli  nilipanga kufanya mkutano na wadau wa maendeleo kujadili changamoto za wananchi wa Temeke haswa wale wanaoishi Kilakala ambao eneo lote limejaa maji, kwenye eneo lile tumelazimika kuweka pump inayonyonya maji lakini tulikuwa na changamoto kama mafuta na mambo mengine hivyo nilikuwa nimepanga kukutana na wadau mbalimbali kwenye ukumbi wa Temeke Executive  lakini ghafla nashangaa nakuja kupewa taarifa nisifanye mkutano wowote kwa vile eti wamesikia nataka kukutana na vijana wa CUF ya Lipumba niwashawishi"- aliongeza Mh. Mtolea.

Mh. Mtolea ameendelea kusikitika kwa kudai kuwa kuzuia vikao kufanyika ni kuwanyima wananchi kutimiziwa haki zao za msingi.

"Mimi huwa ni mstaarabu nikitaka kufanya mkutano huwa nawajulisha jeshi la polisi na wao mara nyingi wamekuwa wakinipatia ulinzi tunashirikiana vizuri lakini hili la leo nilivyoenda kuwataarifu ni kama nimeenda kuwambia nizuieni. Hichi kitendo cha kutubana upinzani naona ndicho kinachoendelezwa zaidi, walitunyima mikutano ya hadhara wakaruhusu mikutano ya kujadili maendeleo na mimi siku zote huwa nafanya hivyo sasa nashangaa wamekuja na hii ya kuzuia vikao vya ndani  bila kuuliza kikao kinahusu nini  na wakati  vinaruhusiwa. Hata kama ni kweli nilikuwa nakutana na watu wa CUF mimi ni Mbunge katiba ya chama inaniruhusu kufanya mkutano kwa sababu tayari kwenye chama nina uongozi"- alimaliza Mh. Mtolea.

LEMA AFICHUA UKATILI WA TRA KWA WAFANYABIASHARA WA ARUSHA

MBUNGE wa Arusha Mjini, Godbless Lema amesema   Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), imekuwa ikiwatesa na kuwasumbua wafanyabishara hasa katika miji mikubwa ya Dar es Salaam, Arusha na Mbeya.

Lema alitoa kauli hiyo bungeni jana wakati akiuliza swali la papo kwa papo kwa Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa.

“Mheshimiwa Waziri Mkuu, tunafahamu jitihada za serikali ya awamu hii ya kupigania sera ya viwanda ambalo ni jambo jema.

“Kila mwenye akili timamu analipongeza ili suala la viwanda liwe na ukweli ni lazima wawekezaji na wafanyabiashara wawe na mazingira bora.

“TRA wamekuwa wakitesa na kusumbua wafanyabishara hasa katika miji mikubwa ya Dar es Salaam, Arusha na Mbeya hasa katika  mkoa ninakotoka, TRA wanatumia polisi, Takukuru na usalama wa taifa kuwatishia katika masuala ya kodi.

“Ili waweze kufanya biashara zao kwa uhakika nini kauli ya serikali juu ya mfumo wa TRA?”alihoji Lema.

Akijibu swali hilo, Majaliwa alisema ni kweli kipo chombo kinachowajibika kukusanya kodi kutoka kwa walipa kodi wakiwamo wafanyabishara.

“Ni kweli wanatambau ulipaji kodi ni wadaiwa sugu, TRA kupitia chombo chake Task Force makao makuu, ilikuwa na mkakati wa kuwapitia wadaiwa sugu. polisi, Takukuru walienda kule kuona hakuna utoaji rushwa.

“Na katika msafara huo kama Arusha, polisi walikuwa wanatumia silaha na utaratibu kama fedha zinaweza kulipwa papo kwa papo na nimshukuru RC wa Arusha kwa kuwaita wafanyabishara na kuwaeleza wale polisi walikuwapo kwa ajili ya kulinda tu na alirudisha amani.

“TRA inao utaratibu, wale ambao wanadhani haiwatendei haki kusikiliza kero watumie madawati hayo kupeleka malalamiko hayo.

“Serikali inawaheshimu wafanyabishara na inatambua umuhimu wao wa kulipa kodi na kila mmoja  atambue wajibu wetu na waendelee kutoa ushirikiano na haiwapelekei hofu,”alisema Majaliwa.

IKULU;Rais Magufuli akubali ombi la Kagame kupeleka walimu wa kiswahili Rwanda!!!

Rais Magufuli leo amepokea ugeni kutoka kwa Rais Kagame wa Rwanda na kuzungumza nao Ikulu, Dar es Salaam.

Rais wa Tanzania Dkt. John Magufuli amepokea barua yenye ujumbe wa Rais wa Jamhuri wa Rwanda Mhe. Paul Kagame iliyowasilishwa kwake na Mjumbe Maalum ambaye ni Waziri wa Elimu wa Rwanda Dkt. Musafiri Papias Malimba.

Pamoja na kupokea barua hiyo, Mhe. Rais Magufuli na Dkt. Musafiri Papias Malimba wamezungumzia masuala mbalimbali ya ushirikiano kati ya Tanzania na Rwanda ikiwemo katika sekta ya elimu hususani maendeleo ya sayansi na teknolojia.

Aidha, Mhe. Rais Magufuli ameipongeza Rwanda kwa kuamua lugha ya Kiswahili ianze kufundishwa katika shule zake na ameahidi kuwa Tanzania ipo tayari kutoa walimu wa kwenda kufundisha lugha hiyo.

WAZIRI MKUU WA ISRAEL AFUNGUKA HAYA JUU YA JPM!!

WAZIRI Mkuu wa zamani wa Israel, Ehud Barak ameipongeza Serikali ya Tanzania kwa jinsi inavyovitunza vivutio vyake vya utalii. Barak anayeongoza kundi la watalii zaidi ya 100 kutoka Israel ikiwamo familia yake, aliwasili nchini mapema wiki iliyopita kwa ajili ya utalii.

Walitembelea Makumbusho ya Olduvai Gorge na kueleza kufurahishwa kwake na jinsi Serikali inavyofanya katika kuhifadhi maeneo ya kihistoria kama Olduvai Gorge. Aidha, walitembelea Hifadhi za Taifa za Ngorongoro na Serengeti zilizoko katika Urithi wa Dunia, unaotambuliwa na Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO).

Meneja Mawasiliano wa Shirika la Taifa la Hifadhi za Taifa (Tanapa), Pascal Shelutete, alisema Waziri Mkuu huyo wa zamani wa Israel alizuru pia Olduvai Gorge akiwa njiani kwenda Hifadhi ya Taifa ya Serengeti alikopokelewa na Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Ramo Makani. Akiwa Olduvai Gorge ambayo ni moja ya eneo maarufu la masuala la kale katika Afrika Mashariki na linalotembelewa kwa kiasi kikubwa na watalii wakienda katika hifadhi za taifa za Ngorongoro na Serengeti, Barak alisema eneo hilo ni muhimu kutokana na uhusiano wake na binadamu wa kizazi cha sasa.

Akiwa na msafara wake waliwasili nchini Jumanne iliyopita wakitumia ndege ya Shirika la Ndege la Israel, na kutua kwenye Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro (KIA) walipokelewa na Waziri wa Maliasili na Utalii, Profesa Jumanne Maghembe. Mapema mwezi huu, Balozi wa Israel nchini, Yahel Vilan alimtembelea Rais John Magufuli na kumueleza kuwa watalii wapatao 200 walikuwa wanatarajiwa kuitembelea nchi mwezi huu.

Tanzania na Israel zimeapa kudumisha uhusiano wake na ulipata nguvu zaidi baada ya uamuzi wa Tanzania kufungua ubalozi wake nchini Israel na kufunguliwa kwa kituo cha Israel cha utoaji viza jijini Dar es Salaam, Novemba mwaka jana. Sekta ya utalii itanufaika kutokana na hatua hizi. Kulingana na taarifa za kuaminika kutoka Bodi ya Utalii Tanzania (TTB), idadi ya watalii kutoka Israel imeongezeka kutoka 3,007 mwaka 2011 hadi 14,754 mwaka 2015.

Waziri Majaliwa Kaagiza Mkurugenzi wa Kampuni ya 4×4 Tanzania Limited Akamatwe

Waziri Majaliwa wa kwanza (kulia) akizungumza jambo.WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amesema timu aliyoiunda ichunguze tuhuma za ubadhirifu kwenye Chama Kikuu cha Ushirika wa Tumbaku (WETCU) imekamilisha kazi yake na imebaini madudu mengi zaidi.
Machi 16, 2017, Waziri Mkuu aliivunja Bodi ya WETCU pamoja na Bodi ya Tumbaku Tanzania (TTB) kwa sababu ya kushindwa kusimamia zao hilo pamoja na matumizi mabaya ya fedha za umma.
Alimuagiza Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Tabora awakamate viongozi wanne wa pamoja na kufunga ofisi za chama hicho hadi uchunguzi wa fedha za chama hicho utakapokamilika.
Waziri Mkuu ambaye amefanya ziara ya siku moja mkoani Tabora, ametoa kauli hiyo leo (Jumamosi, Aprili 15, 2017) wakati akizungumza na wajumbe zaidi ya 300 wa mkutano wa wadau wa zao la tumbaku katika ukumbi wa Kiyungi mwana Isike, mjini Tabora.
“Nilikuja Tabora mara ya kwanza ili kuchukua hatua za dharura na leo nimekuja kuendelea na mkakati wa Serikali ya awamu ya tano wa kuwezesha kilimo cha tumbaku kiwe na tija kwa wakulima na ndiyo maana niliomba wakulima, wanunuzi wa tumbaku, vyama vya msingi vya ushirika (AMCOS) na viongozi wa Serikali wawepo kwenye mkutano huu,” amesema.
Akitoa mrejesho juu ya uchunguzi uliofanywa na timu aliyoiunda, Waziri Mkuu amesema WETCU haikuwa na kitengo cha ununuzi kwa zabuni.
“Waliunda kampuni inayoitwa FDTU (Flu and Dark Tobacco Union) ambayo ni Umoja wa Wenyeviti wa Union zote za Tumbaku nchini ambayo ilipewa kazi zote za ununuzi wa pembejeo na hela walikuwa wanagawana,”amesema.
“Tumefanya ufuatiliaji hadi katika benki lakini kwenye akaunti hakuna hela mpaka sasa. Tumeangalia chanzo cha fedha za union zenu na kubaini hakuna fedha zinazotoka FDTU kwenda WETCU,” ameongeza.
Akifafanua kuhusu kashfa ya ununuzi wa gari aina ya shangingi lenye namba za usajili T181 DEN ambao ulifanywa kinyume na maazimio ya mkutano mkuu, Waziri Mkuu amesema viongozi wa WETCU walitumia zaidi ya sh. milioni 220 kuzidi kiwango kilichoidhinishwa na Mkutano Mkuu cha kununua gari lenye thamani ya sh. milioni 40.
“Gari walilolinunua ni la mwaka 2008 na siyo la mwaka 2015 kama taarifa zinavyoonesha. Lilikwishatumika kwa kilometa zaidi ya 95,000 lakini likarekebishwa hadi kubakiza kilometa 16,000 ili lionekane ni jipya,… maana yake wamekula fedha nyingi sana na ni lazima tuwachukulie hatua za kisheria kwa sababu wamekula fedha, wamenunua gari lililotumika na siyo maamuzi ya mkutano mkuu.”
Waziri Mkuu ameagiza Mkurugenzi wa kampuni ya 4×4 Tanzania Limited, Bw. Faraz Yaseen naye akamatwe na kuhojiwa ni kwa nini alihusika na kuuza gari la mwaka 2008 lakini akabadilisha nyaraka ili lionekane ni la mwaka 2015.
Akitoa ufafanuzi kuhusu uuzaji wa hisa za WETCU, Waziri Mkuu amesema chama hicho kilikuwa na hisa milioni 36 ambapo kilitoa milioni sita ili ziuzwe na zikapatikana sh. bilioni 2.520 na ndiko huko walitoa fedha za kununulia gari na vifaa vya ofisi kwa sh. milioni 49.
“Walichukua hisa 100,000 na kuziuza na wakapata sh. milioni 250 lakini fedha hizo hazikuwekwa kwenye akaunti ya chama. Hisa zilizobakia, ambazo ni milioni 30, walishaanza mchakato wa kuuza hisa milioni 28. Je mliahsatoa kibali Wamempatia cheti halisi cha hisa hizo wakala Zani Security ili auze hisa hizo bila kuomba kibali cha Mkutano Mkuu,” amesema.
“Kwa vile hawakupata idhini ya Mkutano Mkuu, na wala hawakufuata taratibu, kanuni na sheria, kuanzia leo nimesitisha mauzo ya hisa hizo na kirudishwe Tabora mapema iwezekanavyo. Mrajisi fuatilia Zani Securiy warudishe kile cheti kinachowapa dhamana ya kuuza hizo hisa.”
Waziri Mkuu amesema, kwa vile WETCU ina madeni mengi katika benko za CRDB na NMB, viongozi wa chama hicho waliamua kufungua akaunti mpya za fedha za kitanzania na dola za Marekani kwenye benki ya EXIM. Walifungua akaunti ya muda maalum na kuweka huko fedha ambazo zilishalisha faida ya zaidi ya sh. milioni 14 katika kipindi cha miezi mitatu.
“Ninamuagiza Mrajisi wa Vyama vya Ushirika kupitia COASCO (Shirika la Ukaguzi na Usimamizi wa Vyama vya Ushirika) ya Tabora afuatilie benki ya EXIM hapa Tabora ili kubaini ni akina nani walikuwa wakifanya miamala hiyo,” amesema,
Mkutano huo ulihudhuriwa pia na Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Watu Wenye Ulemavu), Mhe. Jenista Mhagama; Waziri wa Kilimo, Mifugo na Uvuvi, Dk. Charles Tizeba; Wakuu wa Wilaya, Wakurugenzi na Wenyeviti wa Halmashauri za mkoa huo.
IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU,
S. L. P. 980,
DODOMA,
JUMAMOSI, APRILI 15, 2017

MAGUFULI AMCHARUKIA KUBENEA!!!



Rais John Magufuli jana alitumia staili nyingine ya kumshtaki kwa wananchi mbunge wa Ubungo, Said Kubenea katika hafla ya uzinduzi wa majengo ya mabweni ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM).

Chuo hicho kipo katika jimbo hilo linaloongozwa na mbunge huyo wa Chadema na hivyo katika hali ya kawaida alitakiwa kuhudhuria sherehe hizo za ufunguzi, lakini Rais Magufuli alipomuulizia ili azungumze chochote kwa niaba ya wananchi wake, hakuwapo.

Hii ni mara ya pili kwa Rais Magufuli kutumia staili hiyo kumchongea mbunge baada ya kufanya hivyo mapema mwezi Machi alipokuwa Kilwa mkoani Lindi.

Siku hiyo, akiwa njiani kwenda mikoa ya kusini kwa ziara ya kikazi, Rais alimtaka mbunge wa Kilwa Kaskazini (CUF), Vedasto Ngombale Mwiru kutoa ahadi ya kuchangia ujenzi wa kituo cha afya kutoka kwenye fedha za mfuko wa jimbo, lakini mbunge huyo aligoma akitoa utetezi kuwa hana fungu hilo.

Jitihada za Rais kumshawishi atoe ahadi hiyo hazikufanikiwa baada ya mbunge huyo kusema hataweza kufanya hivyo kwa sababu fedha za mwaka huu zimekwisha akisisitiza, “msemakweli ni mpenzi wa Mungu.”

Ndipo Rais alipowaambia wananchi kuwa wamemsikia mbunge wao na baadaye kutoa ahadi yake.

CCM Wamteua DR Gertrude Rwakatare Kuchukua Nafasi ya Sophia Simba Aliyefukuzwa


Mchungaji Dkt. Getrude Rwakatare ameteuliwa kuwa Mbunge Viti Maalumu(CCM) kuchukua nafasi ya Sophia Simba aliyefukuzwa uanachama.

Ikumbukwe kuwa kwa mara ya kwanza Mchungaji Rwakatare alipata nafasi kama hii katika Bunge lililopita.

Uteuzi huu umekuja baada ya Spika wa Bunge kuiandikia barua ofisi ya Tume ya Taifa ya Uchaguzi(NEC) na kuiarifu juu ya uwepo wa nafasi ya Ubunge Maalum kwa upande wa Chama Cha Mapinduzi(CCM) baada ya Sophia Simba kupoteza sifa za kuwa Mbunge baada ya kuvuliwa uanachama.

Alichosema Zitto Baada ya Hoja Yake Kutupwa..!!!!

Mbunge wa Kigoma mjini kwa tiketi ya Chama cha ACT Wazalendo Mhe. Zitto Kabwe amesema hajakata tamaa na kukataliwa kwa hoja yake binafsi iliyotaka kuundwe tume ya kuchunguza vitendo vya uhalifu hasa utekaji na uteswaji kwa watu wasiokuwa na hatia. 

Kupitia mtandao wa kijamii, Zitto  amewataka wananchi wawaunge mkono kwenye ajenda ya kuufumua mfumo wa Usalama wa Taifa ili waweze kuunda idara itakayosimamia usalama na maslahi ya taifa badala ya kuteka na kutesa watu.

"Hoja binafsi kuhusu kuundwa Kamati Teule ya Bunge kuchunguza vitendo vya utekaji na uteswaji imekataliwa jana. Hata hivyo, tutaendelea na hoja hiyo wiki ijayo baada ya mapumziko ya Pasaka ambapo waziri mwenye kuhusika na Usalama wa Taifa ataleta hoja ya makadirio ya matumizi ya idara hiyo. Tunataka Idara ya Usalama ifanyiwe marekebisho makubwa ikiwemo kuvunjwa na kuundwa upya. Wananchi tunaomba mtuunge mkono kwenye ajenda hii ya kuufumua mfumo wetu wa usalama wa taifa ili kuunda idara inayosimamia usalama na maslahi ya taifa badala ya Idara ya kuteka na kutesa watu." Ameandika Zitto 

Kwa upande mwingine Mbunge huyo amesikitishwa na matukio yanayozidi kutokea katika nchi huku akisema laiti kama kungekuwa na usalama taifa imara pasingekuwa yanatokea vitendo vya utekaji.
 

Total Pageviews