HABARI ZA TOWN: siasa

~Jamvi La Habari Na Burudani~

Breaking News
Loading...
Showing posts with label siasa. Show all posts
Showing posts with label siasa. Show all posts

Dr Slaa afunguka haya kuhusu ujio wake Tanzania!!!

Image result for dr slaa
Aliyekuwa katibu mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo, Dkt. Willbroad Slaa amesema hana mpango wa kurudi Tanzania kwa sasa na kwamba taarifa zinazosambazwa hazina ukweli wowote.

Slaa alijiuzulu ukatibu mkuu wa CHADEMA na siasa za vyama baada ya CDM kumpokea Edward Lowassa na kumpa nafasi ya kuwakilisha chama hicho katika uchaguzi wa urais 2015

BUNGE LA TANZANIA LAPOKEA UGENI MZITO HUKO BUNGENI DODOMA!!!

unnamedSpika wa Bunge, Mheshimiwa Job Ndugai (kushoto) akisalimiana na Mbunge wa Bunge la Umoja wa Ulaya Mhe. Alojz Peterle (kulia) pale ugeni wa Wabunge kutoka Bunge la Umoja wa Ulaya ulipomtembelea leo katika Ukumbi wa Spika Mjini Dodoma.ASpika wa Bunge, Mheshimiwa Job Ndugai akizungumza jambo pale ugeni wa Wabunge wa Bunge la Umoja wa Ulaya ulipomtembelea leo katika Ukumbi wa Spika Mjini Dodoma.A 1Spika wa Bunge, Mheshimiwa Job Ndugai akizungumza  jambo pale alipopata ugeni wa Wabunge wa Bunge la Umoja wa Ulaya, katika Kikao kilichofanyika leo katika Ukumbi wa Spika Mjini Dodoma.A 4Spika wa Bunge, Mheshimiwa Job Ndugai (wanne kulia) akipiga picha ya pamoja na Wabunge wa Bunge la Umoja wa Ulaya wakiongozwa na Mhe. David Martin (wanne kushoto) baada ya kumalizika kikao kilichofanyika  leo katika Ukumbi wa Spika Mjini Dodoma.A 3Wageni wa Spika wa Bunge, Mheshimiwa Job Ndugai ambao ni Wabunge wa Bunge la Umoja wa Ulaya wakifwatilia Vikao vya Bunge vinavyoendelea leo Mjini Dodoma.

PROF Jay atema cheche bungeni kuhusu vilio vya wasanii.

Mbunge wa jimbo la Mikumi Mh. Joseph Haule amefunguka na kuitaka serikali kuwekeza fedha za kutosha katika Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo ili wizara hiyo iweze kuwekeza katika sanaa na kuacha kuwatumia wasanii kama makarai ya kujengea.

Prof Jay alisema hayo  Bungeni wakati akichangia makadilio ya mapato na matumizi ya Wizara ya Habari kwa mwaka 2017/ 2018 

"Wasanii wa Tanzania wamekuwa katika mazingira magumu sana na wamekuwa katika umasikini mkubwa licha ya mara nyingi kutumiwa katika kampeni mbambali na hata katika chaguzi zilizopita mmeona jinsi wasanii walivyokuwa wakitumika, mmewatumia kama makarai na baada ya hapo mmeyaweka uvunguni, tunajua makarai huwa yanatumika kwenye kujenga maghorofa na vitu vingine lakini nyumba ikikamilika yanawekwa uvunguni hayatakiwa kuonekana hata kwa wageni" alisema Prof Jay 

Mbali na hilo Prof Jay amesema wasanii wengi wa Tanzania wanakuwa masikini sana sababu wakishatumika huwa hawathaminiwa tena na kuachwa mpaka wakati mwingine wa uchaguzi au kampeni 

Maswali magumu yenye majibu magumu kutoka kwa Lipumba haya hapa!!!

 
Profesa Ibrahim Lipumba, ambaye ana mgogoro na chama chake cha CUF, jana alitinga studio za Clouds TV kujibu mapigo ya hasimu wake, Maalim Seif Sharif Hamad katika kipindi cha 360 na mambo matatu yalijitokeza.
Alichukua hatua hiyo baada ya kipindi hicho cha 360 kumuhoji Maalim Seif juzi na kumsukumia lawama Profesa Lipumba kuwa ndiye anayesababisha mgogoro katika chama hicho, akisaidiwa na Serikali.
File:Ibrahim Lipumba.jpgMaalim Seif, ambaye alimtuhumu Lipumba kuwa msaliti, alisema ni bora kukaa meza moja na CCM kuliko mwanasiasa huyo msomi wa uchumi kwa kuwa chama hicho tawala kinajulikana kuwa adui wa CUF hivyo ni rahisi kuchukua tahadhari.
CUF ipo katika mgogoro baada ya Profesa Lipumba kuandika barua ya kujiuzulu wadhifa wake Agosti 2015 kwa kile alichoeleza kuwa nafsi inamsuta na mwaka mmoja baadaye aliandika barua ya kubatilisha uamuzi huo.
Hata hivyo Mkutano Mkuu wa CUF, uliofanyika Hotel ya Blue Pearl jijini Dar es Salaam, haukukubali Profesa Lipumba kurejea madarakani, badala yake ukakubaliana na barua yake ya kujivua nyadhifa zote, hali iliyoanzisha mgogoro na viongozi wenzake.
Katika mahojiano hayo ya jana, Profesa Lipumba alizungumza na kujibu mambo mbalimbali lakini kati ya hayo, masuala matatu yalikuwa na utata zaidi.
Jambo la kwanza ni pale Profesa Lipumba alipoulizwa na watangazaji wa kipindi hicho sababu za kwenda kuhudhuria Mkutano Mkuu wa CUF uliofanyika Agosti 21, 2016 wakati hakuwa mjumbe.
Lipumba alijibu kuwa aliitwa na baadhi ya wajumbe wa mkutano huo ambao alisema walimtumia ujumbe mfupi wa simu na baadhi kumpigia simu.
“Nilipigiwa simu na wajumbe 12 wakiniambia ‘hapa kwenye mkutano mkuu, barua yako (ya kujiuzulu) inasomwa. Sisi wajumbe tunataka uje uthibitishe hii barua ndiyo yenyewe uliyoandika?” alisema Lipumba.
“Nilipata simu kama kumi au kumi na mbili. Nikaamua kwenda kwenye eneo la Mkutano Mkuu.Niliondoka nyumbani mimi na dereva mpaka kwenye Mkutano Mkuu.”
Maelezo hayo yalimfanya mtangazaji aulize sababu za kwenda kwenye Mkutano Mkuu wakati hajaalikwa na si mjumbe wa mkutano huo.
“Ah! Mimi nimeitwa na wajumbe kwamba hapa unahitajika kuja kuthibitisha,” alisema na kupandishiwa swali jingine.
“Hiyo imekaaje kikanuni. Unapotakiwa kuja kuthibitisha, kikanuni imekaaje. Unaalikwa kwa kutumiwa barua?” aliulizwa.
“Hapana nilitumiwa ujumbe wa simu. Katika taratibu zetu sisi ujumbe wa simu, barua ni utaratibu halali kumualika mtu kuhudhuria kikao,” alisema.
“Sasa sikujua nani ana-chair (mwenyekiti) nani katibu wa kikao kile, lakini nimekwenda kwenye mkutano mkuu. Nimefika eneo la mkutano nimekuta vijana, walinzi wa chama, blue guard, Nimeshuka wamenipokea, wakaniingiza ndani ya ukumbi wa Mkutano Mkuu. Wakanipeleka mahali nikaenda kukaa.”
Alisema alikuta mjadala kuhusu aitwe kujieleza, lakini mwenyekiti (Julius Mtatiro) alikataa na baada ya mapumziko, walipiga kura na kutangaza matokeo kuwa waliokuwa wanamtaka Lipumba ni wajumbe 14 na waliomkataa ni 476.
“Hiki ndicho chanzo cha sokomoko kutokea na kusababisha wajumbe kuimba ‘ni heri ya Jecha (Salim Jecha) aliyefuta matokeo kuliko Maalim Seif kutangaza matokeo wakati kura hazikupigwa’,” alisema Profesa Lipumba.
Jecha ni mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi Zanzibar (ZEC).
Mahojiano hayo pia yalijikita katika sababu za uamuzi wa Lipumba kujiuzulu.
Katika mahojiano hayo, Lipumba alisema aliamua kujiuzulu kwa sababu aliona si sahihi kwa Edward Lowassa kuingia ndani ya Ukawa na kugombea urais na kwamba hakuwa kinara wa kumshawishi Lowassa kujiunga upinzani.
“Ni uongo na mimi nilipata taarifa kutoka kwa (mwenyekiti wa NCCR-Mageuzi, James) Mbatia kuwa Lowassa anahitaji kuzungumza na mimi na hata siku moja sikuwahi kuomba niunganishwe naye,” alisema.
Aliongeza kuwa hata siku moja hakuwahi kuomba namba ya Lowassa.
Alipotafutwa jana, Mbatia alisema hawezi kuzungumza chochote kwa sasa kuhusu kinachoendelea ndani ya CUF.
Juzi, Maalim Seif alisema ana ushahidi kuwa Profesa Lipumba alikwenda kumtafuta Lowassa ajiunge na Ukawa na alimuomba Mbatia amuunganishe naye.
Wakati akimkaribisha Lowassa ndani ya Ukawa Julai 2015, Profesa Lipumba alisema suala la ufisadi ni mfumo na si la mtu mmoja mmoja.
“Sisi tunaponda ufisadi na mfumo wa kifisadi na chanzo kikubwa cha ufisadi ni mfumo ndani ya CCM, kwanza tuing’oe CCM, hapo ndipo tutakapoweza kuondoa ufisadi,” alisema Lipumba wakati wa kumtambulisha Lowassa wakati huo.
“Lowassa alikumbwa na tuhuma za ufisadi mwaka 2008, leo ni 2015 lakini ufisadi umeongezeka au umepungua? Lowassa hayupo serikalini? Tatizo ni mfumo na jambo la kwanza ni kuing’oa CCM.”
Lakini jana, Lipumba alisema kuwa hakusema Lowassa ndiye awe kamanda wa kuongoza vita dhidi ya ufisadi.
Hata hivyo, katika mahojiano hayo Profesa Lipumba alikiri kwenda nyumbani kwa Lowassa na kufanya mazungumzo kuhusu watu wanaomuunga mkono kujiunga na Ukawa.
Alieleza kuwa mipango yote ilisukwa na Chadema na kitendo cha yeye kuhusishwa katika mchakato wa kumshawishi Lowassa ulikuwa ni propaganda.
Alisema hatua yake ya kumlaumu Maalim Seif imetokana na katibu huyo mkuu huyo kufanya vikao na Chadema bila kumshirikisha yeye.
Kuhusu nguvu yake ndani ya CUF, Profesa Lipumba alisema baadhi ya wanachama walimfuata kumshawishi ashiriki kampeni kwa kuwa walimtambua kama bado mwenyekiti.
“Walikuja kina mbunge wa Temeke, Abdallah) Mtolea na (mbunge wa Kinondoni, Maulid) Mtulia kuniomba nishiriki kampeni zao, nikawaeleza siwezi kutokana na hali ilivyo kwa kuwa nitaharibu uhusiano kati yao na Chadema,” alisema
Akizungumzia suala hilo jana, Mtolea alithibitisha kuwa alienda kwa Lipumba kumuomba ahudhurie uzinduzi wa kampeni kama mwanachama wa kawaida.
“Nilimuomba akanikatila kwa sababu ya Lowassa. Nikamweleza mkutano ni wangu mimi siyo wa Lowassa akakataa pia,” alisema Mtolea.
Kuhusu kuwa msaliti, Lipumba alisema “waliosaliti ni wale waliofanya utaratibu wa kumleta Lowassa”.
Sababu za kujiuzulu,
Akizungumzia sababu za kujizulu, Profesa Lipumba alisema ni ukosefu wa umoja ndani ya CUF, hasa baada ya Ukawa kuundwa.
Alisema wakati mwingine, vikao vilifanyika bila yeye kupewa taarifa. “Nikajikuta nina wakati mgumu kulinda maslahi ya umoja na maslahi ya chama na ukosefu huu ulitumiwa na Chadema kuwadhalilisha wagombea wa CUF Bara,” alisema.
Alisema Chadema walisema CUF haina fedha za kusimamisha mgombea na taarifa hizo walipewa na Maalim Seif.
Kuingia ofisini
Profesa Lipumba alisema baada ya Ofisi ya Msajili wa vyama vya Siasa kumtambua kama Mwenyekiti alikwenda moja kwa moja hadi ofisi ya makao ya chama hicho, Buguruni na kukanusha kuwa hakuvamia.
Alisema anamtambua Maalim Seif kama Katibu Mkuu, lakini alishangaa kwa nini hafiki ofisini.
Alisema tayari ameshamwandikia barua ya kuitisha kikao cha kamati tendaji kisha Baraza Kuu la Uongozi.
Aliongeza kuwa hakuanza kutofautiana na Maalim Seif baada ya kujiuzulu bali wakati wa mchakato wa maoni ya Rasimu ya Katiba mpya.
Alisema Maalim Seif alitaka muungano wa mkataba wakati msimamo wa chama ilikuwa ni Serikali tatu.
CUF ina wabunge 42, na kati ya hao ni wawili tu wanaomuunga mkono Profesa Lipumba

Mzee Mkapa asema haya kuhusu serikali ya Magufuli na sakata la vyeti feki!!!

Image result for mkapa
Rais mstaafu wa awamu ya tatu wa Tanzania, Benjamin Mkapa kwa mara ya kwanza amezungumzia utawala wa Rais Dkt John Pombe Magufuli huku akimpongeza utendaji kazi wake unavyokwenda.

Rais Mkapa alimpongeza kwa kufanikisha zoezi la kuondoa wafanyakazi hewa na wenye vyeti vya kughushi vya taaluma na kazi, na akasema anasikitika tu kwamba kwa nini yeye hakufanya hivyo wakati wa utawala wake.

Mzee Mkapa aliyesema hayo alipokuwa akifanya mazungumzo yake na Shirika la Habari la Ujerumani (DW) ambapo miongoni mwa mambo mengi aliyozungumzia ni utawala wa Rais Magufuli, uhuru wa vyombo vya habari, masuala ya uchumi.

Alisema Mkapa kuwa, wenye vyeti feki au watumishi hewa walikuwa wakiingizia serikali hasara wengine wakiendelea kukaa madarakani bila ya kustaafu, hivyo lilikuwa ni jambo la lazima kufanyika ni kwa manufaa ya taifa.

“Masikitiko yangu pekee ni kwamba kwa nini sikufanya uhakiki huu wakati nikiwa madarakani. Labda nilikuwa na mambo mengine makubwa zaidi niliyotakiwa kuyafanya lakini kwa hili alilofanya Magufuli namuunga mkono kabisa,” alisema Mkapa.

Kauli hii ya Rais Mkapa imekuja ikiwa ni siku chache baada ya Rais Dkt Magufuli kuwaamuru watumishi wa umma 9,932 waondoke kwenye utumishi wao baada ya kubainika kughushi vyati vyao.

ZITTO AFUNGUKA HAYA MAZITO KUHUSU MDEE!!!

Mbunge wa Kigoma mjini, Zitto Zuberi Kabwe, ametoa shukrani kwa Bunge la Tanzania kwa kumsamehe Mbunge wa Kawe, Halima Mdee kwa kuendelea na vikao vya Bunge.

Mbunge Zitto ametumia ukurasa wake wa Facebook kutoa shukrani hizo kwa bunge. Ameandika hivi:

 Hatimaye Waziri Kivuli wa Fedha ndg. Halima Mdee amesamehewa na ataendelea na vikao vya Bunge. Hii ndio haki. Mtu aliomba radhi hadharani, kwanini aadhibiwe. Shukran Kwa Bunge.

Halima Mdee alituhumiwa kutumia lugha chafu bungeni wakati wa uchaguzi wa Bunge la Afrika Mashariki, Aprili 14 mwaka huu.

NDOTO ZA MAGUFULI KUTIMIZWA!!!

Image result for magufuli
WATANZANIA wameshukiwa na neema katika mwaka huu wa fedha kutokana na Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano kupanga kuunganisha mikoa yote nchini kwa kujenga barabara za lami na madaraja.

Bajeti hiyo ni ya neema pia kwa wakazi wa Dar es Salaam kutokana mkoa huo kupangiwa kiasi kikubwa cha fedha kwa ajili ya kujenga barabara za lami nyingi, za viungio na za juu kwa ajili ya kupunguza msongamano wa magari jijini humo na katika majiji na mji mikubwa mingine.

Bajeti hiyo ya mwaka 2017/18 ya Sh trilioni 4.5 imeweka vipaumbele katika kukamilisha miradi inayoendelea, miradi inayofadhiliwa na washirika wa maendeleo kwa miaka mitano 2016/17 hadi 2020/21, kutekeleza ahadi za ilani ya CCM ya Uchaguzi Mkuu 2015 na ahadi za viongozi wa serikali walizotoa wakati wa kampeni za uchaguzi mwaka juzi.

Akisoma bungeni jana, Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Profesa Makame Mbarawa alisema, bajeti hiyo ya ukombozi kwa maana ya kuwa inalenga kuunganisha mitandao ya barabara nchini ambayo ni muhimu katika kujenga uchumi wa viwanda.

“Bajeti hiyo iliyotengwa katika sekta tatu za wizara hiyo, sekta ya ujenzi itatumia Sh trilioni 1.9 wakati sekta ya uchukuzi ambayo imeongoza kwa kuombewa fedha nyingi inaomba kupewa Sh trilioni 2.6 na mawasiliano Sh bilioni 18.1,” alisema.

Waziri huyo alisema, kati ya fedha hizo, trilioni 2.6 zilizoombwa kwa ajili ya sekta ya uchukuzi, kiasi cha Sh bilioni 900 zitatumika katika kujenga Reli ya Kati sehemu ya Dar es Salaam hadi Dodoma kwa kiwango cha standard gauge.

Profesa Mbarawa alisema, pia Sh bilioni 500 zitatumika katika kampuni ya ndege kwa ajili ya kukamilisha malipo ya ununuzi wa ndege tatu ambapo mbili za aina ya CS 300 zenye kubeba abiria 127 kila mmoja na moja ya masafa marefu aina ya Boieng 787-8 Dreamliner yenye uwezo wa kubeba abiria 22.

Kuhusu Sekta ya ujenzi iliyotengewa Sh tril 1.9, Prof Mbarawa alisema Sh bilioni 12.8 zitatumika kwa ajili ya kufidia ili kupata eneo kwa ajili ya ujenzi wa barabara ya Dar es Salaam- Chalinze Km 144, ujenzi ambao utakuwa wa ushirikiano baina ya serikali na sekta binafsi (PPP).

Waziri Mbarawa alisema, kati ya fedha za sekta hiyo, Sh bilioni 30, zitatumika katika kujenga barabara za mikoani na madaraja ikilenga katika kuunganisha mikoa yote Tanzania kwa barabara za lami.

“Kazi zilizopangwa kutekelezwa ni ukarabati wa km 469.5 kwa kiwango cha changarawe, kujenga km 58.4 kwa kiwango cha lami na madaraja 12,” alisema. Alisema kati ya fedha hizo, Sh bilioni 46.9 zimetengwa kwa ajili ya kuendelea na ujenzi wa flyover ya Tanzania, Interchange ya Ubungo pamoja na upembuzi yakinifu na usanifu wa kina kuboresha barabara za makutano.

“Barabara hizo ni iliyopo eneo la Kamata, Magomeni, Mwenge, Tabata/Mandela, Morocco, Buguruni, Makutano ya barabara za Kinondoni/ Ali Hassan Mwinyi na Kenyatta na Selander zinapokutana barabara ya Mwinyi na Umoja wa Mataifa (UN),” alisema.

Alisema, pia fedha hizo zitatumika katika kuboresha viwanja vya ndege kikiwamo cha Kimataifa cha Kilimanjaro kilichotengewa Sh bilioni 32.6 kwa ajili ya upanuzi wa barabra ya kuruka na kutua ndege.

“Fedha zitatumika kujenga maegesho ya ndege, barabara za viungio, jengo la abiria na ujenzi wa barabara mpya ya kiungio, usimikaji wa taa za kuongozea ndege na ujenzi wa mfumo mpya wa majitaka,” alisema.

Profesa Mbarawa alisema, Uwanja wa Ndege wa Kimataifa cha JNIA umetengewa Sh blioni 35 kwa ajili ya kuendelea na ujenzi wa jengo jipya la abria terminal III na miundombinu yake.

Sekta ya mawasiliano imepata Sh bilioni 18.1 kidogo ukilinganisha na sekta nyingine mbili, fedha hizo pia zitatumika katika kuendeleza ujenzi wa mkongo wa Taifa hadi katika makao makuu ya wilaya zote nchini.

“Zitatumika pia katika ujenzi wa vituo viwili vya kutunza data kimoja Dodoma na kingine Zanzibar pamoja na kuwezesha uwekezaji wa viwanda nchini,” alisema. Kuhusu Mfuko wa Barabara, Waziri Mbarawa alisema, unatarajia kukusanya Sh bilioni 917.5 ambazo zitatumika katika kufanya matengenezo ya barabara nchini, katika fedha hizo sekta ya ujenzi imetengewa Sh bilioni 642.3 na ofisi ya Rais Tamisemi Sh bilioni 275.2.

Kati ya Sh bilioni 642.3 zilizotengwa, Sh bilioni 573.1 kwa ajili ya Tanroads na Sh bilioni 63.7 kwa ajili ya sekta ya ujenzi kufanya matengenezo ya barabara za wizarana Sh bilioni 5.52 kwa ajili ya uendeshaji wa Bodi ya Mfuko wa Barabara.

Mbarawa alisema, miradi ya barabara kuu itaendeshwa kutokana na fedha kutoka mfuko wa barabara, ambapo Sh bili 16.3 zimetengwa kwa ajili ya kufanya upembuzi yakinifu na usanifu wa kina kilometa 3,624.8.

“Miradi ya barabara za mikoa imetengewa Sh bilioni 33.9 kutoka katika mfuko wa barabara, fedha hizo zitafanya kazi ya ukarabati wa barabara kilometa 688.3 kwa kiwango cha changarawe na kujenga kilometa 40.6 kwa kiwango cha lami na madaraja 12,” alisema.

Waziri Mbarawa alisema, jumla ya Sh milioni 573.1 kutoka mfuko wa barabara zitatumika kwa ajili ya matengenezo ya barabara kuu, barabara za mikoa, madaraja uendeshaji mizani, gharama za usimamizi na uendeshaji wa wakala wa barabara.

MSIGWA AGEUKA MBOGO BUNGENI DODOMA!!!

Mbunge wa Iringa Mjini (Chadema), Mchungaji Peter Msigwa 

Dodoma. Mbunge wa Iringa Mjini (Chadema), Mchungaji Peter Msigwa ameitaka Serikali ieleze sababu za kuwatumbua watumishi bila ya kuwapa nafasi ya kujitetea.

Hata hivyo, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais (Utumishi na Utawala Bora) Angella Kairuki alikana madai hayo akisema hakuna mtu anayetumbuliwa bila ya kufuata utaratibu.

Katika swali la nyongeza, Msigwa alitaka kujua haki za watumishi wanaotumbuliwa kwa kile alichokiita kwa mafungu, lakini bila ya kuwapa nafasi ya kujitetea.

Pia, alihoji wanatakiwa kutafuta haki yao wapi hata kama wametumbuliwa na Rais.

Katika swali la msingi, Mbunge wa Viti Maalumu (Chadema), Ruth Mollel alitaka kujua ikiwa Tanzania inaongozwa kwa kuzingatia Katiba, sheria na kanuni ni kwanini baadhi ya watumishi walioajiriwa wamekuwa wakisimamishwa kazi na Rais, wakuu wa mikoa na wilaya bila ya kuzingatia sheria ya utumishi wa umma na kanuni zake.

Akijibu, Waziri alisema kanuni za utumishi wa umma hutekelezwa kwa kuzingatia katiba, sheria, kanuni, utaratibu na miongozo na kwa mujibu wa ibara ya 36 ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano ya mwaka 1977, Rais ndiye mwenye mamlaka ya mwisho kuhusu usimamizi na uendeshaji wa utumishi wa umma.

Alisema ibara ya Katiba imempa uwezo Rais wa kukasimu madaraka mbalimbali kwa ndani ya utumishi lakini kukasimu huko hakuwezi kutafsiriwa kuwa Rais hana mamlaka hayo tena kama ilivyofafanuliwa katika ibara 36 (4) ya Katiba na Kifungu cha 21 (4) na Sheria ya Utumishi wa Umma Sura ya 298.

Kairuki alisema hata watumishi waliofukuzwa au kusimamishwa kazi na Rais, wana nafasi ya kukata rufaa kwa mamlaka zingine na ikibainika kuwa walionewa, watapewa haki yao.

Katika majibu ya nyongeza, Waziri wa Nchi Ofisi ya Tamisemi, George Simbachawene alisema wakuu wa mikoa na wilaya wanayo mamlaka lakini wanapotoa uamuzi wa kuwasimamisha kazi watumishi, huwa si mwisho bali wakurugenzi ndiyo hutakiwa kuchukua hatua au makatibu tawala wa mikoa.

RAIS SHEIN AWEKWA KITIMOTO BUNGENI DODOMA!!!

MSEMAJI Mkuu wa Kambi rasmi ya Upinzani bungeni, Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano), Ally Saleh jana alisusa kuendelea kusoma hotuba yake kwa madai kuwa hakuna uhuru wa kujieleza katika chombo hicho cha kutunga sheria.

Saleh alikatiza hotuba hiyo, baada ya kutakiwa kufuta kauli iliyohoji uhalali wa Dk. Ali Mohammed Shein kukalia kiti cha Rais wa Zanzibar.

Mwanasheria Mkuu wa Serikali( AG), George Masaju alisema maneno yaliyotamkwa na Saleh hayapo katika uhalisia.

Masaju alisema Saleh anapaswa kurekebisha kauli yake kwa sababu Rais Dk. Shein alishinda uchaguzi mkuu uhalali.

Kufuatia ushauri wa AG, Mwenyekiti wa Bunge, Mussa Hassan Zungu alisema maneno yaliyomo katika hotuba ya upinzani yaliyosomwa na mbunge Saleh ni lazima ayatoe kwa sababu siyo maneno sahihi na hayapo katika uhalisia.

“Kwa hiyo maneno katika ukurasa wa tatu, kwenye namba tatu inatoka, kwa Dk. Shein inatoka kwa sababu alichaguliwa kihalali, ukurasa wanne wote," alisema Zungu.

Hata hivyo Mbunge Saleh aliamua kuondoka bila ya kuendelea kusoma hotuba hiyo na kusema kuwa uhuru katika bunge hauko kiasi cha kutosha.

Mbali na kuhoji uhalali wa Rais wa Zanzibar, wakati akisoma hotuba hiyo Saleh alidai wizara zinakiona cha moto, mawaziri wamebanwa mbavu na kwamba muungano siyo ajenda ya awamu ya serikali ya awamu ya tano kutokana na matendo ambayo yanatokea.

Alisema endapo hali hiyo itaendelea basi "kidagaa kitamuozea mtu mkononi na maiti atampakata yeye."

Mara baada ya kusoma sehemu hizo katika hotuba yake, ndipo Mwanasheria Mkuu Masaju aliposimama na kutoa taarifa na kusema kuwa Saleh anatumia maneno ambayo ni makali.

Masaju alisema Saleh anapaswa kurekebisha kauli kwa sababu hakuna wizara iliyokiona cha moto wala waziri aliyebanwa mbavu, pia Rais Dk. Shein alishinda uchaguzi mkuu kwa uhalali.

Kauli hiyo ya Masaju ilizua tafrani bungeni hali iliyosababisha baadhi ya wabunge upinzani kusimama na kuomba taarifa.

Mbunge wa Kawe (Chadema), Halima Mdee alisema Mwanasheria Mkuu Masaju anapoteza muda kwa kuwa anazungumzia masuala ambayo hayapo kikanuni.

Naye Mbunge wa Iringa mjini (Chadema), Peter Msigwa alisema uhuru wa kambi ya upinzani upo kikatiba.

Alisedma bunge linaendeshwa kwa kanuni hivyo walio wachache wasikilizwe na walio wengi wanapswa kutoa maamuzi.

“Sasa Serikali hata sisi tuliowachache tunavyotoa maoni na mawazo tunazuiwa, hivi utamaduni wa bunge hili ni upi? AG badala ya kuisaidia Serikali ili inyooke amekuwa mtetezi, na bado anapotosha hapa," alisema Msigwa.

"Sisi ni upinzani na ndiyo kazi yetu, sasa kama kila kitu tunachoandika tunapingwa, mnataka tufanyeje? Hatujaja hapa kuwasikiliza nyie.”

FEDHA KIDOGO
Wakati akisoma taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Viwanda, Biashara na Mazingira kuhusu utekelezaji wa majukumu ya hifadhi na usimamizi wa mazingira katika ofisi ya Makumu wa Rais, mjumbe wa kamati hiyo Marry Mwanjelwa alisema ofisi hiyo ilipewa fedha kidogo kulinganisha na maombi ya mwaka 2016/17.

Alisema kati ya Sh. bilioni 20.3 zilizoidhinishwa na bunge kwa mwaka 2016/17 kwa matumizi ya ofisi ya Makamu wa Rais Mazingira hadi Machi 15 ni Sh. bilioni 7.79 tu zilikuwa zimetolewa.

Awali wakati akiwasilisha bungeni makadirio ya mapato na matumizi kwa mwaka wa fedha 2017/18, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais, January Makamba aliomba bunge kuidhinisha makadirio ya matumizi ya Sh. bilioni 15 kwa ajili ya wizara yake.

Kadhalika alisema kwa mwaka 2017/18 ofisi ya Makamu wa Rais Mazingira iatendelea kuratibu mashirikiano yatakayoiwezesha Zanzibar kujenga uwezo na kunufaika katika shughuli za uchimbaji wa gesi na mafuta.

Alisema katika mwaka 2016/17 Serikali ya Mapinduzi Zanzibar (SMZ) imeendelea kupokea fedha kutoka Serikali ya Muungano wa Tanzania, na kwamba hadi kufikia mwezi uliopita Sh. bilioni 1.4 za mfuko wa maendeleo ya jimbo na Sh.bilioni 15.75 za kodi ya mishahara zilipokelewa na SMZ.

IKULU;RAIS MAGUFULI AFANYA UTEUZI HUU MWINGINE!!!

Rais John Magufuli amemteua Profesa Raphael Chibunda kuwa Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo (SUA).

Taarifa iliyotolewa na Katibu Mkuu Kiongozi Balozi John Kijazi, Ikulu Jijini Dar es Salaam jana imeeleza kuwa uteuzi wa Profesa Chibunda unaanza jana tarehe 24 Aprili, 2017.

Kabla ya uteuzi huo Profesa Chibunda alikuwa Mkurugenzi Msaidizi, Idara ya Sayansi na Teknolojia katika Wizara ya Elimu, Sayansi, Teknolojia.

Profesa Raphael Chibunda anachukua nafasi ya Profesa Gerald Monela ambaye amemaliza muda wake.

Wakati huo huo, Rais Magufuli amewasili mjini Dodoma ambako pamoja na mambo mengine atakuwa mgeni rasmi katika sherehe za maadhimisho ya miaka 53 ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar.
 

Total Pageviews